80. Liko Neno Moja Nipendalo
1. Liko Neno moja nipendalo,
ni chakula cha moyo;
Neno hili linanituliza
nikipatwa na shida:
Kumtazama Bwana wetu pale,
atoapo jasho kama damu,
akubalipo mzigo,
Baba aliomtwika.
2. Siku zote namkumbuka yeye,
alivyosulibishwa,
akivumilia taabu kimya
kama mwana wa kondoo.
Nami akanikumbuka mimi,
akisema: Yamemalizika!
Huko aliniteka,
nami niwe mtu wake.
3. Bwana wangu,
u mwenye huruma,
mimi ni mkosaji tu;
nilipokuwapo penye giza
wewe ukatokea,
ukamtafuta kondoo wako,
kabla mimi sijakusikia.
Watoa ukombozi unipao uhuru.
4. Ndimi huru lako, Bwana Yesu,
wewe ndiwe Bwanangu.
Jina lako, bora liung’aze moyo
wangu vizuri.
Amani yako nikae nayo,
siku zangu zote mpaka kufa.
Ndivyo ninavyoomba,
Bwana unikubali.
Comments
Post a Comment