81. Ulimwengu Tazama

1. Ulimwengu tazama,

   Yesu Mwokozi wako 

   asulibiwavyo. 

   Mwenye heshima yote 

   anayavumilia

   mateso tena matusi.


2. Karibia tazama 

   maungo yake yote 

   yatokavyo damu.

   Na moyo wake mwema 

   kwa shida na uchungu 

   unaugua vigumu.


3. Nani akupigaye, 

   aliyekufanyia 

   mambo kama haya? 

   Wewe huna makosa 

   kama wengine wote,

   hujui kosa lolote.


4. Makosa yangu mimi 

   yaliyo kama mchanga, 

   hayahesabiki,

   ndiyo yakutiayo 

   mateso na uchungu  

   uliyoyavumilia.


5. Mimi nimestahili 

   kulipa haya yote, 

   na kufungwa sana. 

   Mapigo na mateso 

   uliyopata wewe

   yalitoka kwangu mimi.


6. Umejitwika mzigo

   ulio mzito sana  

   kuliko jiwe kuu. 

   Wachukua maovu, 

   tupate kuokoka 

   tukae nawe daima!

Comments

Popular posts from this blog

18. Umati wa Yesu

2. Hosiana, Mesiya