83. Yesu, Kuteswa Kwako

1. Yesu kuteswa kwako 

   nitakufikiri.

   Nipe kwa shauri hili

   roho na mbaraka. 

   Moyo wangu uone 

   hali yako Yesu,

   jinsi ulivyoteswa 

   kwa ajili yetu.

 

2. Moyo wangu uone 

   taabu yako kubwa, 

   maumivu, mapigo,

   na kuwambwa mtini, 

   taji lako la miiba 

   tena misumari, 

   iliyokuumiza, 

   hata kufa kwako.

 

3. Nikitazama yote 

   yaliyokutesa, 

   nifikiri sababu 

   na maana yake. 

   Sababu ndio mimi 

   na makosa yangu: 

   umepata mateso, 

   nipate huruma.


4. Yesu unifundishe 

   nijute kwa moyo; 

   nisikuzidishie 

   shida na uchungu. 

   Nisiweze kupenda  

   yaliyokutesa: 

   nataka kuyaacha 

   na kukufuata.   

Comments

Popular posts from this blog

18. Umati wa Yesu

2. Hosiana, Mesiya