87. Ee, Watoto Njooni

1. Ee, watoto njooni,

   njooni Golgota,

   mtazameni Yesu aumizwavyo!


2. Mtazameni huko 

   mkamtazame, 

   Sogeeni kwake, ametupenda.


3. Sogeeni kwake, mkamtazame,

   mioyo iyeyuke, mwangukieni!


4. Mioyo imlilie anayeteswa;

   mzigo wetu mkubwa aukubali.


5. Mzigo wa makosa 

   ya ulimwengu. 

   Mpeni nanyi nyote

   mioyo yenu!


6. Apata mshahara, ni kufa kwake; 

   wewe una raha, kwake ni kufa.


7. Ataona enzi ya utukufu. 

   Tuimbe  Haleluya 

   na kumshukuru. 

Comments

Popular posts from this blog

18. Umati wa Yesu

2. Hosiana, Mesiya