88. Nataka Kusimama

1. Nataka kusimama

   chini ya msalaba,

   kama kivuli cha mwamba

   wakati wa mchana,

   kama ni maji nyikani,

   kambi safarini,

   na hapa nitapumzika,

   kwani jua kali. 


2. Mahali pema sana 

   chini ya msalaba, 

   kwani hapo ninaona 

   upendo wa Yesu. 

   Yakobo alivyoona 

   ndotoni zamani,

   mti Yesu aliowambwa, 

   ni ngazi kwa Mungu.


3. Juu ya msalaba huo

   Yesu alikufa. 

   Alikufa tuokoke, 

   tuliopotea.

   Ninastaajabu kabisa 

   ni mambo mawili:

   Kwake Yesu ni upendo, 

   kwangu mimi kosa!


4. Wataka kuonana

   na Yesu mbinguni, 

   yakupasa kukaa kwanza chini 

   ya mti huo.

   Ni kweli siku chache tu mateso

   na shaka.

   Halafu pasipo mwisho 

   furaha kwa Bwana!

Comments

Popular posts from this blog

18. Umati wa Yesu

2. Hosiana, Mesiya