89. Kumbuka Getsemane
1. Kumbuka Getsemane,
asongapo Shetani,
Mwokozi ukamwone
ateswavyo shambani;
nao uchungu wewe,
aombapo kumbuka!
2. Kumbuka barazani
ashtakiwapo Yesu;
mtazame Bwana huko,
walipomhukumia;
upate soni wewe,
mti wa Yesu kumbuka!
3. Kumbuka na Golgota
alipokufa Bwana.
Upaji wa tambiko
ameutoa Yeye.
Kasema: Imekwisha
Mti wa Yesu kumbuka!
4. Kumbuka bustanini
walipomzika Yesu,
kukiwa bado giza.
Mfu amekwenda wapi?
Amefufuka Yeye;
Ufufuko kumbuka!
Comments
Post a Comment