9. Faraja, Tumaini Langu
1. Faraja, tumaini langu
usiniache gizani.
Moyo ni wazi kukungoja,
Ee Yesu uniingie.
Furaha ya mbingu na
nchi, Mwana Adamu na Mungu;
Ee nuru kutoka mbinguni, an-
gaza moyo wangu huu.
2. Mtoto mpendwa,
nakuomba, chagua moyo
wangu huu, ufanye kuwa hori
lako ukalazwe humo wewe.
Ili nipate mwisho mwema
wa shida yangu na vita.
Zaliwa ndani yangu Yesu,
na ndani yangu ukue.
3. Mwokozi wangu utulize,
tumaini hili kubwa.
Ukija nitakupokea
kwa roho nyenyekevu, hii.
Uweza wangu wote
pia wakungojea kwa
uchu. Nataka
kukutumikia:
Njoo, Yesu usikawie.
Comments
Post a Comment