94. Unipe Nguvu Bwana
1. Unipe nguvu,
Bwana nikumbuke
mateso yako yaliyokupata,
kutukomboa tulioanguka
katika dhambi.
2. Umemtii Baba,
mpaka kufa kwako
mahali petu ulisulibishwa,
makosa yetu yalikuwa
mengi, umetufia.
3. Wokovu wangu ulinitafuta;
nakuangukia Mwokozi wangu,
nakushukuru nikiitazama
huruma yako.
Comments
Post a Comment